Kaimu
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Ally
Malewa(pichani) amefanya Mabadiliko ya Uongozi kwa baadhi ya Wakuu wa
Magereza Mikoa na vituo mbalimbali hapa nchini.
Mabadiliko
hayo ni pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Katos Rugainunura amehamishiwa
Makao Makuu ya Magereza sehemu ya Utawala na nafasi yake inakaimiwa na
Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Mzee Nyamka aliyekuwa Mkuu wa Utawala
Magereza Mkoani Morogoro.
Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Antonino Kilumbi aliyekuwa Mkuu wa
Magereza Mkoa wa Dodoma amehamishwa kwenda Makao Makuu ya Magereza kuwa
Mkuu wa Kikosi cha Ujenzi na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Julius Sang’udi aliyekuwa Mkuu wa
Magereza Mkoa wa Mbeya.
Aliyekuwa
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP
Anderson Kamtiaro anaenda kuwa Afisa Mnadhimu Magereza Mkoani Arusha na
nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Hassan
Mkwiche ambaye alikuwa ni Mkuu wa Gereza Kuu Karanga, Moshi.
Aliyekuwa
Mkuu wa Gereza Same Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Evarist Katego
anakwenda kuwa Mkuu wa Gereza Kuu Karanga, Moshi. Aliyekuwa Mkuu wa
Magereza Mkoa wa Mwanza Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP
Uwesu Ngarama amehamishiwa Makao Makuu kuwa Boharia Mkuu wa Jeshi na
nafasi yake inachukuliwa na aliyekuwa Afisa Mipango wa Jeshi ACP Athuman
Kitiku.
No comments:
Post a Comment