Sunday, January 8, 2017

Basi la Mohammed Trans Laua Watatu na Kujeruhi Watano Singida

SeeBait
Matukio ya ajali za barabarani yameendelea kuutikisa Mkoa wa Singida baada ya abiria 10 kupoteza maisha na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa ndani ya siku tisa. 
Desemba 30, mwaka jana katika Kijiji cha Tumuli Wilaya ya Iramba abiria watatu walikufa na wengine 25 kujeruhiwa na ajali nyingine ilitokea Januari Mosi katika Kijiji cha Kintukuntu wilaya humo na kuua abiria mmoja na kujeruhi watatu. 
Ajali nyingine iliyohusisha bajaji ilitokea jana  Januari 7 katika Barabara ya Mwankoko na  kumuua dereva na abiria wawili. 
Siku moja kabla ya tukio hilo, ajali ya basi la Mohammed Trans lililokuwa linatokea Tanga kwenda Shinyanga ilisababisha vifo vya abiria watatu na kujeruhi wengine watano wote wakiwa ni walimu. 
Akitoa taarifa ya ajali ya basi la Mohammed Trans jana, Kaimu Kamanda Polisi mkoani hapa, Mayala Towo alisema ilitokea Januari 6, saa nne usiku katika Kijiji cha Mseko wilayani Iramba. 
Kamanda huyo aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Mussa Rajabu (55), Farahan Manyama (34) na John Tungaraza (39) wote wakiwa ni walimu, wakazi wa Geita. 
Pia, alisema majeruhi ambao pia ni walimu wamelazwa katika hospitali ya wilaya hiyo. 
Kamanda huyo aliongeza kuwa walimu hao walikuwa wametokea kwenye Chuo cha Eckenford mkoani Tanga walikokuwa wakichukua mafunzo mbalimbali. Alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva. 
Towo alisema basi hilo lenye namba za usajili T 786 AWJ aina ya Scania lilikuwa linaendeshwa na Jovin Jackson (38), mkazi wa Shinyanga liligonga kwa nyuma lori lenye namba B.6705A lililokuwa likivuta tela B.0568A lililokuwa likienda Burundi. 
Akifafanua, alisema dereva wa basi alitaka kulipitia lori hilo, lakini alipogundua hataweza aliamua kurudi ghafla kushoto na mwendo kasi aliokuwa nao alijikuta analigonga lori hilo kwa nyuma. 
Towo alisema baada ya kusababisha ajali hiyo dereva alitoroka na kukimbilia kusikojulikana. Juhudi zinaendelea kumsaka ili afikishwe mahakamani.

Diamond kufunika ufunguzi wa Kombe la Mataifa ya Afrika ‘AFCON 2017’

Ule wimbo unaosikika mtaani wa ‘pesa kupotea mifukoni’ haumhusu Bosi wa WCB, Diamond Platinumz anayeendelea kuzihesabu ‘deals’ kubwa zaidi za matukio ambayo dunia nzima inayaangalia kwa macho yote.

Siku chache baada ya kutumbuiza kwa ustadi mkubwa kwenye tuzo za CAF jijini Abuja nchini Nigeria, Diamond amealikwa kutumbuiza kwenye ufunguzi wa Kombe la Mataifa ya Africa 2017 (AFCON 2017), Januari 14 nchini Gabon.

Chibu Dangote amewapa habari hiyo njema mashabiki wake kupitia mitandao ya twitter na Instagram, kwa kupost taarifa ya show yake hiyo iliyowekwa kwenye akaunti maalum ya AFCON 2017.

“GABON!!! You know we gat to make a World History on the 14th January right?? See you this this Coming Weekend then…👈 #WcbWasafi” aliandika.

Saturday, January 7, 2017

DART

     Dar es Salaam — The arrival of the long awaited Dar es Salaam Bus Rapid Transit (Dart) was greeted with jubilation by most of the city dwellers who have been struggling with transport issues.
Since they started operating on Tuesday by giving free rides across the city, some of the passengers have refused to alight from the vehicles giving the crew hard time.
It is evident that the excited passengers who are not going to any specific destination are enjoying the back and forth rides. Users are also struggling to master the use of special electronic 
 cards to board the buses.


Commuters in Dar es Salaam on Wednesday started using special rapid shuttle buses connecting the city centre with its outskirts.
Early risers looking forward to beat the morning gridlock to town with the rapid shuttles were however disappointed as the buses started running from 10 am.

Kaimu kamisha jenerali wa magereza afanya mabadiliko ya uongozi kwa maafisa waandamizi wa magereza

Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dkt. Juma Ally Malewa(pichani) amefanya Mabadiliko ya Uongozi kwa baadhi ya Wakuu wa Magereza Mikoa na vituo mbalimbali hapa nchini.

Mabadiliko hayo ni pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Katos Rugainunura amehamishiwa Makao Makuu ya Magereza sehemu ya Utawala na nafasi yake inakaimiwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Mzee Nyamka aliyekuwa Mkuu wa Utawala Magereza Mkoani Morogoro.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Antonino Kilumbi aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma amehamishwa kwenda Makao Makuu ya Magereza kuwa Mkuu wa Kikosi cha Ujenzi na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Julius Sang’udi aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mbeya.

Aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Anderson Kamtiaro anaenda kuwa Afisa Mnadhimu Magereza Mkoani Arusha na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Hassan Mkwiche ambaye alikuwa ni Mkuu wa Gereza Kuu Karanga, Moshi.
Aliyekuwa Mkuu wa Gereza Same Kamishna Msaidizi wa Magereza ACP Evarist Katego anakwenda kuwa Mkuu wa Gereza Kuu Karanga, Moshi. Aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mwanza Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza SACP Uwesu Ngarama amehamishiwa Makao Makuu kuwa Boharia Mkuu wa Jeshi na nafasi yake inachukuliwa na aliyekuwa Afisa Mipango wa Jeshi ACP Athuman Kitiku.

Lowassa, Maalim Seif Kutikisa Zanzibar Kesho

Wanasiasa wakongwe nchini, Maalim Seif Sharif Hamad aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Edward Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika, kesho wanatarajia kuungana kwa mara ya kwanza jukwaani tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Vigogo hao wa vyama vya CUF (Maalim Seif) na Chadema (Lowassa) wataunguruma katika viwanja vya Skuli ya Fuoni visiwani Zanzibar kumnadi mgombea ubunge wa jimbo la Dimani kwa tiketi ya CUF, Abdulrazaq Khatib Ramadhani, katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Januri 22 kuziba nafasi ya aliyekua mbunge wa jimbo hilo, Hafidh Ally Tahir aliyefariki dunia Novemba 11  mwaka jana.

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu  amesema kuwa chama chake kimemua kuungana na CUF katika uchaguzi huo ili kuhakikisha mshirika wake huyo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) anamshinda mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Aidha, Mwalimu aliongeza kuwa baada ya Lowassa kushiriki uzinduzi wa kampeni hizo kesho, viongozi wengine wa Chadema watafuata kwa kufanya mikutano mbalimbali jimboni humo. Alisema kuwa baada ya Lowassa atafuata Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe pamoja Tundu Lissu kwa nyakati tofauti, kisha wengine wataendelea hadi mwisho wa kampeni hizo.

Akizungumzia uamuzi huo wa Chadema, Mkurugenzi wa Habari,Uenezi na Mawasiliano kwa Umma, Salim Bimani alieleza kufurahishwa na uamuzi huo wa Chadema na kueleza kuwa hatua ya Lowassa kuhudhuria uzinduzi huo itaongeza hamasa kubwa kwa wapenzi wa chama hicho.

“Umenambia hadi Lowassa atakuwepo? Ni furaha iliyoje, Wanzibari wana shauku kumuona. Siku ya kampeni patakuwa hapatoshi Skuli ya Fuoni, hapa Simba (Maalim Seif) kule Lowassa kipenzi kingine cha Wazanzibar,” Bimani anakaririwa na Mwananchi.

Aliongeza kuwa kama Lowassa atahudhuria mkutano huo atakuwa na mambo mawili makubwa ya kufanya, la kwanza likiwa kuwashukuru Wazanzibar kwa kura walizompa katika uchaguzi Mkuu wa mwaka jana. Na la pili litakuwa kumpigia kampeni mgombea wa CUF, Abdulrazaq Khatib Ramadhani.

Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Maalim Seif ambaye ni Katibu Mkuu wa CUF, wataingia katika jimbo hilo ikiwa ni siku chache baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kufanya uzinduzi wa kampeni hizo akiambatana na viongozi wengine wa kitaifa wa chama hicho.

Hivyo, kwa muktadha wa kisiasa, vigogo hao wa Ukawa wana kazi ya kusawazisha matuta yaliyowekwa na timu ya chama tawala iliyoongozwa na Kinana.

Zitto Kabwe Aitaka Serikari itangaze balaa la njaa


Kiongozi wa Chama cha ACT –Wazalendo, Zitto Kabwe ameitaka Serikali kutangaza rasmi baa la njaa kwa mujibu wa sheria kutokana na hali ya chakula kuwa mbaya nchini.

Kauli ya Zitto imetolewa wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisisitiza utunzaji wa chakula baada ya kukagua maghala ya nafaka yanayomilikiwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Kanda ya Songea.

Agizo la Majaliwa pia limetolewa siku mbili baada ya Waziri wa Kilimo, Dk Charles Tizeba kutofautiana na Zitto kuhusu hali ya chakula ambapo Waziri huyo alisema hali ya chakula nchini ni shwari huku Mbunge huyo wa Kigoma Mjini akisema ni mbaya.

Jana, mbunge huyo akihutubia mkutano wa kampeni ya kumnadi mgombea udiwani Kata ya Nkome, Geita aliendelea kupigilia msumari kauli yake akisema, “Hali ya chakula ni mbaya, ni mbaya, ni mbaya.”

Alisema baada ya ziara ya Waziri Mkuu kwenye maghala ya Taifa na kujionea hali ya chakula nchini, ni vyema Serikali ikachukua hatua.

“Ninapendekeza Serikali ichukue hatua muhimu ya kisheria ya kutangaza baa la njaa nchini. Tamko la baa la njaa litaisaidia Serikali kupata bajeti ya dharura ya kununua chakula na kutoa uhuru kwa wakuu wa wilaya kutangaza bila woga kuwa maeneo yao yana njaa,” alisema Zitto huku akimpongeza Majaliwa kwa ziara hiyo.

Thursday, January 5, 2017

Infrastructure development to boost economy

    Tanzania has embarked on implementation for construction of six flyovers in Dar es salaam, aiming to decongest the city
    The country is currently facing the challenges of congestions

 in order to address that we are planning to build atleast six flyovers and overheads roads,"the Tanzania national Road agency (TANROADS) chief executive officer, Mr. Patrick Mfugale said, adding that six areas have been identified where there are road junctions










             Prepared by
        1.MICHAEL  E BWELI           2016-04-09853
        2.ELIADA MWAMILIMA      2016-04-09989
        3.JACKSON  E. CHALO         2016-04-09800
        4.KICHUNGA PETER             2016-04-10053
        5.FABIAN    PETER                 2016-04-09770